GLORIOUS CELEBRATION - FAMILY DINNER.
Usiku
wa Jumamosi ya tar. 20/04/2013 ulikuwa ni usiku wa GLORIOUS CELEBRATION
- Family Dinner. Kusudi kubwa lilikuwa ni kukutana na waimbaji wote wa
GC kwa pamoja na wazazi wao, walezi na ndugu wa karibu. Hii pia
ilijumuisha wanandoa kwa wana GC amabao wameoa au kuolewa.
Kwanza tunamshukuru Mungu kwa kibali na yote yaliyojiri. Pili tunamshukuru mlezi na mbeba
maono wa GC, wazazi na wote waliofika. Kwa nyakati tofauti, mlezi wetu
pamoja na baadhi ya wazazi walitoa mahusia mbalimbali. Kwa hakika
ulikuwa usiku wa furaha kuwaona wanaGC kuwa pamoja na wazazi wao, ndugu
jamaa na marafiki.
Ni matumaini yetu siku si nyingi tutakuwa na
usiku wa wanaGC wote, yaaani pamoja na wewe. "Tazama jinsi ilivyo vema
na kupendeza ndugu wakikaa pamoja kwa umoja ni kama mafuta mafuta mazuri
yatiririkayo kichwani mpaka kwenye ndevu za haruni" Zaburi 133:1-2.
SIFA NA UTUKUFU KWA MUNGU
Mr and Mrs Mwakang'ata |
Mama wa mwimbaji wa Gc (Joel lwaga) |
Gc Acapella |
Wazazi wa Acapella |
Wazazi wa Joel |
George Lyanga (mwenyekiti wa Gc) |
Joel Lwaga |
Mc |
GC-Dancers |
msosi
|